KURUGENZI YA CHIPUKIZI WA INJILI

Kurungenzi ya Chipukizi wa Injili (CWI) inahudumia watoto na vijana chipukizi (teenagers) wa Kanisa la EAGT. Lengo kuu la Kurugenzi hii ni kuwaandaa na kuwanoa watoto na vijana chipukizi kukua katika maadili ya Kimungu, kumtumikia Mungu, kufanikiwa katika masomo yao, kuwa wanafamilia bora, na kuwajengea uwezo wa kufanya kazi kujitegemea kiuchumi. Kupitia mafundisho ya Neno la Mungu, mafundisho ya stadi za kazi, ushauri na maombi, watoto na vijana chipukizi wengi wamefaidika na Kurungenzi hii. Kurungenzi ya CWI inatekeleza falsafa ya "Mlee mtoto katika njia impasayo, naye hataiacha atakapokuwa mzee". Kurugenzi hii ina uongozi kuanzia ngazi ya Taifa, Kanda, Jimbo na Kanisa la mahali pamoja. Kauli mbiu ya Kurungenzi hii ni "Tunaanza na Mungu, tunachipuka na Injili, mpaka tutakapokuwa wazee".

Wafuatao ni Viongozi wa Kitaifa wa Kurungenzi ya CWI wanaohudumu katika kipindi hiki:

Jina Cheo Namba ya Simu Barua-pepe ya Ofisi Barua-pepe Binafsi
Rev. Dr. Winfrida James Rwezaura Mkurugenzi - Taifa +255 754 888 137 Mkurugenzi.CWI-Taifa@eagt.or.tz Winfrida.Rwezaura@eagt.or.tz
Mwj. Ezekiel Maliasili Kupasya Makamu Mkurugenzi - Taifa +255 755 993 541 Makamu.Mkurugenzi.CWI-Taifa@eagt.or.tz Ezekiel.Kupasya@eagt.or.tz
Rev. Gidion Jackson Bushize Katibu - Taifa +255 746 153 457 Katibu.CWI-Taifa@eagt.or.tz Gidion.Bushize@eagt.or.tz
Rev. Jaspar Eliyeti Irigo Mhazina - Taifa +255 766 348 003 Mhazina.CWI-Taifa@eagt.or.tz Jaspar.Irigo@eagt.or.tz