The Evangelistic Assemblies of God(T)

EAGT ina imani moja ya Mungu Mmoja nafsi tatu; biblia moja,katiba moja na sasa dira moja! .

"HABARI NJEMA IMEWAFIKIA WATU WOTE"

Dira Yetu

Habari Njema Imewafikia Watu Wote.

Dhima

Kuwa Kanisa moja lenye nguvu za kiroho za kutenda, kumiliki na kuwafikia maelfu ya watu kwa Neno la Mungu, tukiwafundisha kuyashika yote aliyosema Yesu Kristo ili kuwa na Jamii imara iliyofanikiwa kiroho, kiafya, kifikra, kiuchumi, na mambo yote na hatimaye wateule wapate Uzima wa Milele.

Kauli Mbiu

Habari njema kwa wote.

"Tunarudisha utukufu wote, heshima na shukrani kwa Mungu kwa kutujalia mavuno haya. Tangu Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) ilipoanza huduma yake katika taifa hili, chini ya uongozi wa hayati Mch. Dkt. Moses Samuel Kulola, uongozi wa Kanisa umeendelea kuimarishwa kuanzia ngazi ya kitaifa hadi Kanisa la Mahali Pamoja. Katika kuimarisha na kuboresha huduma yake, EAGT inaendelea kusimama imara katika kushikilia Neno la Mungu na inaongozwa na katiba iliyoasisiwa juu ya Tamko la Imani la dhehebu na misingi yake mikuu ya mafundisho."
Dkt. Brown Abel Mwakipesile(Askofu Mkuu)

Kuhusu Kanisa

Kanisa hili linajulikana kwa jina la "The Evangelistic Assemblies of God Tanzania(EAGT)". Kanisa la EAGT ni dhehebu la Kipentekoste nchini Tanzania, linalojulikana kwa msisitizo wake katika uamsho, mafundisho ya kweli na uinjilisti. Makao makuu yake yako Dodoma, na linafanya kazi katika nchi nzima pamoja na nje ya nchi. Soma Zaidi ......

Viongozi Wetu Mahiri

Mungu amelijalia Kanisa la EAGT kuwa na Viongozi mahiri, wenye maono makubwa na msimamo thabiti wa kiroho. Pichani ni Askofu Mkuu wa EAGT, Mch. Dkt. Brown Abel Mwakipesile (katikati); akiwa pamoja na Katibu Mkuu, Mch. Dkt. Leonard Mwizarubi (kulia kwake); Makamu Askofu Mkuu, Mch. Dkt. Joshua Wawa (kushoto kwake); Mhazina Mkuu, Mch. Dkt. PrayGod Mgonja (mwisho kulia kwake); na Mshauri Mkuu, Mch. Dkt. Livingstone Denes Maniyanguru (mwisho kushoto kwake).

6000+
Idadi ya Makanisa
469+
Idadi ya maaskofu
6000+
Wachungaji
"Kanisa langu-EAGT yetu":Habari njema kwa wote"
Zaidi Kuhusu EAGT