The Evangelistic Assemblies of God(T)

EAGT ina imani moja ya Mungu Mmoja nafsi tatu; biblia moja,katiba moja na sasa dira moja! .

"HABARI NJEMA YA WOKOVU IMEWAFIKIA WENGI NCHINI TANZANIA NA NJE YA NCHI"

Dira Yetu

Habari njema ya wokovu kuwafikia watu wote nchini Tanzania na nje ya nchi.

Dhima

Kuwa Kanisa moja lenye nguvu za kiroho za kutenda, kumiliki na kuwafikia maelfu ya watu kwa Neno la Mungu, tukiwafundisha kuyashika yote aliyosema Yesu Kristo ili kuwa na Jamii imara iliyofanikiwa kiroho, kiafya, kifikra, kiuchumi, na mambo yote na hatimaye wateule wapate Uzima wa Milele.

Kauli Mbiu

Habari njema kwa wote.

"We return all glory, honor, and thanksgiving to God for granting us these harvests. Since the Evangelical Assemblies of God Tanzania (EAGT) began its ministry in this nation, under the leadership of the late Rev. Dr. Moses Samuel Kulola, the leadership of the Church has continued to be firmly established from the national level down to the Local Church. This has been achieved through an orderly structure comprising the Archbishop, Regional Bishops, province Bishops, and Local Church pastors, together with their respective offices. In strengthening and improving its ministry, EAGT remains steadfast in upholding the Word of God and is governed by a constitution founded on the denomination’s Statement of Faith and core doctrinal principles"
Dkt. Brown Abel Mwakipesile(Askofu Mkuu)

Kuhusu Kanisa

Kanisa hili linajulikana kwa jina la "The Evangelistic Assemblies of God Tanzania(EAGT)". Kanisa la EAGT ni dhehebu la Kipentekoste nchini Tanzania, linalojulikana kwa msisitizo wake katika uamsho, mafundisho ya kweli na uinjilisti. Makao makuu yake yako Dodoma, na linafanya kazi katika nchi nzima pamoja na nje ya nchi. Soma Zaidi ......>>

Viongozi Wetu Mahiri

Mungu amelijalia Kanisa la EAGT kuwa na Viongozi mahiri, wenye maono makubwa na msimamo thabiti wa kiroho. Pichani ni Askofu Mkuu wa EAGT, Mch. Dkt. Brown Abel Mwakipesile (katikati); akiwa pamoja na Katibu Mkuu, Mch. Dkt. Leonard Mwizarubi (kulia kwake); Makamu Askofu Mkuu, Mch. Dkt. Joshua Wawa (kushoto kwake); Mhazina Mkuu, Mch. Dkt. PrayGod Mgonja (mwisho kulia kwake); na Mshauri Mkuu, Mch. Dkt. Livingstone Denes Maniyanguru (mwisho kushoto kwake).

6000+
Idadi ya Makanisa
469+
Idadi ya maaskofu
6000+
Wachungaji
"Kanisa langu-EAGT yetu":Habari njema kwa wote"
Zaidi Kuhusu EAGT